Recent Articles
Home » Posts filed under video
Showing posts with label video. Show all posts
Showing posts with label video. Show all posts
Monday, December 30, 2013
Tuesday, December 24, 2013
Saturday, December 21, 2013
Friday, December 20, 2013
Jokate, Jacob Stephen, Irene Uwoya, Single Mtambalike, Adam Kuambiana, Stela Mjata, Mzee Ibrahim, Hashim Kambi na Bi Star...hebu tuache masihara jamani, kuna jina la star gani ambalo halipo hapo? Kuanzia wale wa kizazi kileee, hadi hiki cha sasa?
Vichwa hivi adhimu, vinakutana katika mzigo huu unaokwenda kwa jina la Mikono Salama. Tunajua hali ilivyo katika magereza zetu nyingi nchini, sasa inakuwaje mtu ajihisi yuko salama wakati yuko gerezani? Kwanini hasa iwe hivyo? Onja uhondo hapa wakati unasubiri mzigo kamili kushuka hivi karibuni
Ikiwa takriban wiki moja sasa toka mzigo wetu mpya unaokwenda kwa jina la "Bado Natafuta uingie madukani, tumeendelea kupokea ujumbe na simu kutoka kwa mashabiki wetu waliosambaa sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi, wakiulizia ni lini filamu ya DANIJA itaingia madukani.
Ikumbukwe kuwa, filamu hizi mbili zilikuwa zikitangazwa kwa pamoja, na ni wazi mashabiki wetu wengi walitarajia kuwa huenda zingetoka kwa pamoja, lakini kumbe haijawa hivyo.
Tunapenda kuwashukuru kwani hii yote imekuwa ikionyesha kiasi gani mnatupa support ya kutosha na kutuhamasisha kuendelea kufanya kazi kwa minajili ya kuwapatia furaha ambayo mnaitarajia toka kwenye kazi zetu. Na kupitia taarifa hii, tunapenda pia kuwaeleza kuwa, filamu ya DANIJA haijaingia rasmi sokoni, ingali iko kwenye hatua za mwisho za kuingizwa sokoni na panap[o majaaliwa, mwezi januari itakuwa sokoni.
Ikiwa kuna shabiki yetu yeyote ambaye labda amekuwa akisikia kuwa filamu hii iko madukani, au akabahatika kuiona mahali, tunaomba awasiliane nasi haraka kwani hiyo si nakala halali ya kazi yetu kwasababu kazi yetu bado haijaingia sokoni.
Tunawashukuru kwa kuzidi kutuunga mkono na wakati tunaendelea kuisubiri, hapa ni sehemu tu ya uhindo utakaokuwa ukipatikana humo
Wednesday, December 18, 2013
Friday, October 11, 2013
Saturday, October 5, 2013
"Anayejua kumega vikubwa, shurti pia ajue na kulima... wakati unanigeuza geuza kama chapati, ulikuwa unakenua meno, ukijiona umefika..."Unajua nini chanzo cha haya yote? Na mwisho wake ulikuwa nini? Usiwe na shaka, kwani majibu ya maswali haya yote yapo ndani ya mzigo mpya unaokwenda kwa jina la DANIJA.
Kama ilivyo kawaida yetu, hakuna kuremba. Ni mwendo wa kazi zaidi tukiwa tunatambua kuwa unahitaji nini haswa, na ndio sababu tunapenda kukuweka mkao wa kula kwa ajili ya kushuhudia mambo makubwa ndani ya filamu hii.
Moyo wangu ulikuwa mbali lakini uliendelea kutambua uwepo na thamani ya mapenzi yangu kwako. Moyo huu huu uliweza kugusa wa kwako wakati hauna kitu, Na moyo huu huu ndio umerudi tena kwa mara nyingine kukukumbusha mateso uliyapata, Na mateso uliyokuwa unasikia wakati uko mbali na mie
Moyo wangu umekubali kusamehe...
Naam, ni chini ya kampuni mahiri yenye kikosi cha watu wenye kujua nini mashabiki wanapenda, Jerusalem Films Company, hapa akiwepo mwanadada mahiri Shamsa Ford ambaye wala hatuhitajiki kueleza sifa zake maana kila mmoja anazijua, pale kuna Gabo, Patcho Mwamba na wakali wengine kibao.
Ni katika BADO NATAFUTA. Unajua nini kinatafutwa? Tizama utangulizi wa picha hii hapa kisha ujiandae kwa uhondo uliokamili hivi karibuni
Moyo wangu umekubali kusamehe...
Naam, ni chini ya kampuni mahiri yenye kikosi cha watu wenye kujua nini mashabiki wanapenda, Jerusalem Films Company, hapa akiwepo mwanadada mahiri Shamsa Ford ambaye wala hatuhitajiki kueleza sifa zake maana kila mmoja anazijua, pale kuna Gabo, Patcho Mwamba na wakali wengine kibao.
Ni katika BADO NATAFUTA. Unajua nini kinatafutwa? Tizama utangulizi wa picha hii hapa kisha ujiandae kwa uhondo uliokamili hivi karibuni
Tuesday, October 1, 2013
Subscribe to:
Posts (Atom)











